Kampuni ya Vodacom imejitosa kumaliza tatizo hilo kwa wateja wake ambapo kwa kushirikiana na Idara inayosimamia usafiri wa reli na barabara,uongozi wa kituo cha Gautrain,makampuni ya Bombela na Strategic kwa pamoja makampuni hayo yanafanya mchakato wa kumaliza tatizo la mawasiliano katika kituo hicho.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Ukuzaji Teknolojia wa kampuni ya Vodacom Afrika ya kusini Andries Delport anasema “Siku zote nilikuwa nakerwa na kukosekana mtandao wa mawasiliano ya simu na internet kwenye vituo vya treni vlivyopo ardhini hali ambayo imekuwa ikiwasababishia usambufu abiria.Tunajivunia kuwa mtandao wetu mkubwa nchini Afrika ya Kusini tumeamua kumaliza tatizo hili kwa wateja wetu”
Tatizo hili litamalizika kutokana na vifaa bora vya mawasiliano vilivyofungwa na Vodacom katika vituo vitatu vya treni za ardhini,vifaa hivyo vya kisasa ambavyo ni pamoja na antenna za kurusha mawasiliano zimeunganishwa na mkongo wa mawasiliano uliopo eneo la Rosebank na hatua hii pia itawezesha upatikanaji wa huduma za internet kwa urahisi.
“Utekelezaji huu ni wa awamu ya kwanza tukimaliza hatua hii tutajenga mtandao wa mawasiliano chini ya ardhi njia yote inayopita treni na kuhakikisha mawasiliano yanakuwa mazuri muda wote,tuko katika mazungumzo ya awali na wadau tutakaoshirikiana nao kutekeelza mradi huu wa kuboresha mawasiliano kwenye miundo mbinu ya usafri iliyojengwa chini ya ardhi”.Alisema Delport.
Post a Comment